Australia ndiyo mstari wa mbele kabisa katika utekelezaji wa mfumo wa Kura Mbadala (AV), tazama Kura Mbadala, katika matumizi. Mfumo huo ulitangulizwa na serikali ya Kitaifa nchini Australia katika mwaka wa 1918 ili kubadilisha uliokuwepo wa FPTP, tazama Kwanza Baada ya Kura (FPTP), baada ya kudhihirika wazi kuwa magombea wengi wahafidhina waliokuwa wakigombea nyadhifa katika nafasi hizo wangegawa kura zao chini ya mfumo huo wa Kwanza- Baada ya Uchaguzi, hivyo basi kupeana mamlaka kwa vikosi madhubuti vya Chama cha Leba. Kuanzishwa kwake hivyo basi ulihusishwa moja kwa moja na haja ya kukabili uwezekano wa kura kugawika katika na kuhimiza na kuinufaisha miungano kati ya vyama. Uwezo huu wa kuunganisha nia zilizofanana, badala ya kuzigawa, kwa muda mrefu (haijatambuliwa pakubwa) kama sifa ya siasa za uchaguzi nchini Australia, japo haijafanyika hadi katika siku za hivi juzi kwamba uwezo mpana wa kusambaza mapendekezo kama ala ya kuchochea uundaji sera na umewekwa wazi.
Kuna tofauti muhimu kati ya sura mbili za AV ambazo ni “mapendeleo kamilifu” na “mapendeleo ya kuchaguliwa”. Ikiwa uamuzi wa kutumia mapendeleo hayo zaidi ya teuo la kwanza unaachiwa mpigakura, badala ya kulazimishwa, basi mgombea anayeshinda anapaswa kupata kura nyingi katika uchaguzi, japo si lazima ziwe katika zile zilizopigwa. Katika kura amabazo mapendeleo hayawezi kuachiwa mgombea aliyemamlakani wakati huo huchukuliwa kuwa “chakavu”. Kinyume na hayo, nchini Australia, ni hitaji la kisheria kwa mapendeleo yote kuzingatiwa ili kupiga kura halali. Athari kuu ya hili ni kwamba vyama husambaza kadi za “jinsi ya kupiga kura” kwa wafuasi wao siku ya uchaguzi, hivyo kuwapa pendeleo la chama kuhusu mpangilio wa wagombea wote ambalo kisha linaweza kunakiliwa kwenye karatasi ya kura na wapigakura wenyewe, ambao wengi wao hufanya hivyo tu.
Wachanganuzi kuhusu siasa za Australia kihistoria walionekana kuutazama mfumo wa AV kama tofauti na FPTP, hivyo basi katika hali nyingi kutoa matokeo ambayo yalikaribiana sana na mfumo huo katika matokeo ya uchaguzi na muundo wa mfumo wa chama. Douglas Rae, kwa mfano, katika kazi yake ya warsha kuhusu athari ya sheria za uchaguzi, alieleza wazi kuwa “mfumo wa Australia hujitokeza tu kama ulio fomula ya eneo la mtu mmoja”. Wachanganuzi wengine wametetea kuwa kura za mapendeleo hutokeza tofauti ndogo sana na matokeo ya uchaguzi wa Australia na hayajakuwa muhimu katika kudhihirisha jinsi serikali zinavyojengwa.
Kipengele sawa kinachopatikana katika maelezo haya yote ni uwazi kwamba yaliegemea sana kwenye chaguzi za majimbo ya Australia ya miaka ya 1950 na 1960 ambako, kando na wajibu wa Chama cha Kidemokrasia cha Leba (LDP), usambazaji pendwa ulikuwa na athari ndogo sana kwenye matokeo. Hivi sasa mapendeleo hayo huwa na nafasi muhimu katika kuamua matokeo ya uchaguzi wa Australia zaidi ya ilivyokuwa katika miongo iliyopita. Haiwezekani kuchukulia kwamba uteuzi wa kimsingi wa wapigakura utarudiwa vivyo hivyo chini ya mfumo wa FPTP, lakini ingekuwa hivyo basi matokeo ya chaguzi za miaka 1961, 1969, na 1990 yangekuwa kinyume. Kudorora kwa mfumo uliokuwa imara wa vyama viwili, kuimarika kwa vyama vidogo, na kuongezeka kwa athari wagombea binafsi kumeathiri upigaji kura wa mapendeleo kwa kuuimarisha katika miaka ya 1990 kuliko wakati mwingine siku za awali. Jedwali la 1 linaonyesha idadi ya viti ambavyo mapendeleo yamekuwa muhimu katika kuamua matokeo. Sehemu ya pili ni asilimia ya viti ambavyo mshindi wake hakushinda kwa kupendelewa mwanzoni, na hivyo ilitoa matokeo tofauti kushinda yale ambayo yangekuwa chini ya mfumo wa FPTP.
Jedwali la 1: Idadi ya Viti Pale ambapo Mapendeleo yalikuwa mengi na Matokeo Kubadilika, 1963-1996
|
Mwaka wa uchaguzi
|
Mapendeleo (%)
|
Matokeo yaliyobadilika (%)
|
|
1963
|
19.2
|
6.6
|
|
1966
|
25.0
|
4.0
|
|
1969
|
32.0
|
9.6
|
|
1972
|
39.2
|
11.2
|
|
1974
|
26.0
|
7.9
|
|
1975
|
18.9
|
5.5
|
|
1977
|
36.2
|
3.1
|
|
1980
|
32.0
|
4.8
|
|
1983
|
24.8
|
1.6
|
|
1984
|
29.7
|
8.8
|
|
1987
|
36.5
|
2.7
|
|
1990
|
60.1
|
6.1
|
|
1993
|
42.2
|
8.2
|
|
1996
|
39.2
|
4.7
|
Kama jedwali linavyoashiria, takribani nusu ya viti vyote katika chaguzi za hivi karibuni vimeathiriwa na migao ya mapendeleo, ingawa katika visa vingi idadi ya washindi “waliotoka nyuma” kushinda kwa misingi ya mapendeleo ni ndogo, takribani asilimia sita katika miaka ya 1990. Hata kiasi kidogo tu hata hivyo, kingetosha kubadilisha serikali katika chaguzi nyingi.
offering policy concessions on key issues and arguing that the Labor Party was far closer to their core interests than the major alternative, the Liberal/National coalition. This strategy was markedly successful: with minor party support levels at an all time high of around 17 percent, the ALP was the beneficiary of around two-Tatus of all preferences from Democrat and Green voters - a figure which probably made the difference between it winning and losing the election. This was thus a "win-win" situation for both groups: the ALP gained government with less than 40 percent of the Kwanza-preference vote, while the minor parties, which did not win lower house seats, Hata hivyo saw their preferred major party in government and committed to favourable policies in their areas of concern.
Mfano wa kigrafia wa kura za mapendeleo zilizoathiri moja kwa moja uteuzi wa serikali uliofanyika katika uchaguzi wa majimbo wa mwaka wa 1990, ambapo mgombea mtetezi wa Chama cha Leba cha Australia (ALP) alikuwa akisajili matokeo mabaya na alielekea kushindwa katika uchaguzi huo, na pale ambapo uungwaji mkono wa vyama vya kisiasa vya kati kama vile Wanademokrasia na Wanakijani wa Australia ulifikia viwango vya juu. ALP, kutokana na shinikizo la mratibu mkuu Seneta Graham Richardson, walivutia kwa uangalifu kura za kijani, kisiri kwa njia ya mahusiano na makundi ya kutetea mazingira na moja kwa moja kupitia kwa vyombo vya habari kwa wapigakura watarajiwa wa wanakijani, huku wakiomba mapendeleo ya pili au tatu ya wafuasi wa vyama vidogo, hivyo basi kutoa makubaliano ya kisera kuhusu masuala nyeti na kutetea kuwa Chama cha Leba kilikuwa karibu na maazimio yao kushinda
Ili kuona jinsi aina hii ya pendeleo ilivyofanya kazi, mtu anapaswa tu kuchunguza ushindi wa Neville Newell wa ALP katika kiti cha Richmond katika uchaguzi wa majimbo wa mwaka wa 1990. Newell alipata asilimia 27 tu ya kura katika pendeleo la kwanza la kura. Mgombea wa muungano, na aliyekuwa kiongozi wa Chama cha Taifa (NP) wakati huo, Charles Blunt alipata asilimia 41 ya mapendeleo ya kwanza, na alionekana kukaribia kunyakua ushindi kwa njia rahisi. Hata hivyo, hesabu ya kura ilisajili mchanganyiko wa vyama vidogo na Huru, hasa mgombea wa kupinga nyukilia Helen Caldicott, kuingia katika kikosi cha Newell na kumsaidia kushinda kiti kwa asilimia 50.5 ya kura zote za mapendeleo hayo.
Jedwali la 2: Mfano: Hesabu ya Kura katika Chaguzi za Majimbo za miaka ya 1990
Newell alishinda kiti kwa sababu aliweza kupata zaidi ya 77% ya mapendeleo ya Caldicott alipotengwa katika hesabu ya saba. Caldicott mwenyewe alikuwa amepokea wingi wa mapendeleo kutoka kwa wagombea huru. ALP katika Richmond, kama ilivyokuwa katika viti vingine, ndicho kilichonufaika kutokana na hatua hiyo iliyolenga kuimarisha sio tu kura zake bali kuimarisha mapendeleo yaliyopokelewa kutoka kwa wengine: mkakati wa “pendeleo la pili”. Kadiri uungwaji mkono wa Wanademokrasia wa KiAustralia na wale kijani ulipoimarika katika mwaka wa 1990, ndivyo kampeni zenye uangalifu kwa mfumo wa pendeleo la pili ulivyopata thuluthi-mbili ya mapendeleo kutoka kwa vyama hivi, hali iliyoonekana kuamua ushindi wao katika uchaguzi.
Kufaulu kwa mikakati ya ALP katika mwaka wa 1990 kulidhihirika kwa sababu kihistoria mchakato wa kuhamisha mapendeleo hayo umeonekana kunufaisha vyama visivyo vya Leba kushinda ALP. Mfumo wa AV umekuwa na athari mbili kuu chanya kwa vyama visivyo vya Leba: ulichangia katika uundaji wa muungano kati ya vyama Liberal na Nchi (kwa sasa vya kitaifa) kwa kuviwezesha vyote viwili kuweka wagombea katika viti vingine bila hatari ya kugawa kura, na uliwezesha mapendeleo ya chama kimoja kidogo, DLP, kupata umaarufu dhidi ya ALP na kusaidia pakubwa muungano huo kudumisha serikali katika miaka ya 1960. ALP ilipochukua uongozi katika mwaka wa 1983, sera yake ilikuwa kudumisha mfumo wa AV, lakini maelezo ya mapendeleo hayakuwa ya lazima badala yake yalikuwa ya kuteua.
Mfumo wa AV wa Kuteua
Mfumo wa AV wa kuteua unafanana na ule wa kamilifu ila kwamba wapigakura hawahitajiki kutokeza pendeleo kwa kila mgombea; wakitaka, wanaweza kudhihirisha pendeleo lao kwa mmoja. Kwa mujibu wa kauli ya Waziri Mkuu Gough Whitlam, mfumo wa upigaji kura wa kuteua “ndio hatua ya kipekee ya uchaguzi duniani unaoruhusu wapigakura kudhihirisha umoja wao kwa wagombea.” Uchunguzi wa kitaifa wa mwaka 1979 ulionyesha kuwa idadi kubwa ya wapigakura wa Australia walipendelea mfumo wa kuteua, huku asilimia 72 ikiunga mkono wa kuteua na asilimia 26 pekee ikipendelea mfumo wa lazima. Ubora mmoja wa wazi wa mfumo wa kuteua ni kwamba matatizo ya kura zilizoharibika kutokana na makosa ya kuweka nambari ambayo mara nyingi hutokana na mfumo kamilifu. Kwa sababu hii, pendeleo la kuteua ndilo hasa mfano wa pekee wa AV iliyo na uwezo kutekelezwa katika mazingira ya elimu duni na kukosa uwezo wa kuandika nambari.
Mfumo wa kuteua wa AV sasa hivi hutumiwa kwa kura za majimbo katika Wales Kusini Mpya, ambako mfumo huo ulianzishwa na serikali ya Wran Labor mwaka wa 1981, na katika Queensland, ambako ulianzishwa mwaka wa 1992 kutokana na mapendekezo ya Tume ya Uchaguzi na Marekebisho ya Usimamizi, ambayo ilichukulia kuwa kutekeleza kwa ukamilifu upigaji kura kuliwalazimisha wapigakura kudhihirisha pendeleo lao kwa wagombea ambao ufahamu wao kuwahusu ulikuwa mdogo. Kiwango cha “kudondoka” kwa mgombea mmoja pekee, bila kuonyesha mapendeleo mengine, kimeongezeka baada ya muda katika visa vyote viwili. Uamuzi wa kuonyesha mapendeleo pia huonekana kama unaohusiana kwa karibu na mapendekezo yaliyotolewa na vyama kwenye kadi zao za “jinsi ya kupiga kura”. Katika uchunguzi uliofanywa kwenye chaguzi ndogo katika mwaka wa 1992, asilimia 75 ya wapigakura walifuata mielekeo ya vyama, hivyo basi kusababisha asilimia 43 ya viwango vya udondokaji katika eneo moja (Gordon) na asilimia 63 katika jingine (Kuring-gai). Katika kisa cha Kuring-gai, chini ya asilimia 33 ya wapigakura walijaza katika nafasi zote za karatasi ya kura. Katika Queensland, viwango vya udondokaji vilisalia kuwa asilimia 23 kwenye uchaguzi wa kwanza wa OPV mwaka wa 1992, japo vilikuwa juu katika visa vingine ambako nyenzo za jinsi ya kupiga kura kutoka kwenye mojawapo wa vyama vikubwa havikupendekeza mapendeleo. Kuna kipengele cha wazi cha kipekee kuhusu viwango vya udondokaji, ambavyo vinaashiria miungano inayodumu kati ya vyama vya Liberal na National: katika NSW na Queensland. Wapigakura wa Leba wana uwezekano mkubwa wa kudondoka kushinda wafuasi wa vyama vilivyo kwenye muungano.
Athari za AV
Nchini Australia, mavutio katika mfumo wa kupiga kura huelekea kuongezeka kutokana na ubinafsi wake. Athari ya mapendeleo kwenye matokeo ya uchaguzi yameongezeka wazi katika miongo ya hivi karibuni na imekuwa na mchango mkubwa hasa katika ushindi wa chama cha Leba mwaka wa 1990. Kufeli kwa kura ya Wanademokrasia katika mwaka wa 1993 na kuanguka kwa Muungano katika uchaguzi wa majimbo wa mwaka 1996 kulimaanisha kwamba athari za kuenea kwa mapendeleo kuna umuhimu mdogo kuanzia wakati huo, ingawa kumechangia uchaguzi wa idadi ya wagombea huru (wawili katika mwaka wa 1993, watano katika mwaka wa 1996), ambao hushinda viti vyao kwa kupiku wagombea wa chama kikuu kuhusu mapendeleo.
Tathmini ya athari za AV nchini Australia zimeonekana kuegemea kwenye athari za kibinafsi. Wachanganuzi wengine wameuona mfumo huo kama chombo cha kudumisha utawala wa vyama viwili vikuu, ALP na Muungano wa Liberal/National, na cha kubana wajibu wa vyama vidogo katika bunge la chini hadi kwenye kuchochea ujenzi wa sera za vyama vikubwa kuliko kushinda uchaguzi vyenyewe. Wengine hudai kuwa unaweza kuzidisha mamlaka na nafasi ya vyama vidogo, hasa ikiwa vina uwezo wa kushikilia usawa wa mamlaka kati ya vyama viwili vikuu.
Kuna makubaliano makubwa kwamba mfumo wa AV umechangia kuimarika muungano kama vile kati ya vyama vya Liberal na National, na kwamba husaidia wagombea wa kati na vyama, hivyo kuchochea ujenzi wa sera za wastani na kutafuta nafasi sawa. Usemi mkali na chokozi kuhusu siasa za Australia mara nyingi kumetatiza waangalizi dhidi ya kutambua jinsi mienendo ya ushirikiano iliyopo kati ya vyama – kupitia kwa njia ya kubadilishana mipango, kwa mfano – na jinsi vyama vikubwa vinavyokaribiana kuhusiana na maswala mbalimbali ya kisera. Mfumo wa uchaguzi wa AV hutoa kichocheo kwenye mielekeo hii funge.
Maelezo:
[1] Kutoka: Hughes, C.A. na Graham, B.D. (1968), Kijitabu cha Serikali na Siasa za Australia, 1890-1964, Matbaa ya Chuo Kikuu cha Kitaifa cha Australia, Canberra; Hughes, C.A. (1977), A Kijitabu cha Serikali na Siasa za Australia,1965-1974, Matbaa ya Chuo Kikuu cha Kitaifa cha Australia, Canberra; Hughes, C.A. (1986), Kijitabu cha Serikali na Siasa za Australia, 1975-1984, Matbaa ya Chuo Kikuu cha Kitaifa cha Australia, Sydney; Hughes, C.A. (1997), "Maeneo Tenge ya Uchaguzi" katika C. Bean, S. Bennett, M. Simms na J. Warhurst (eds), Siasa za Kuadhibu: Uchaguzi wa Majimbo wa Australia mwaka wa 1996, Allen & Unwin, Sydney, pp. 166-167.
[2] Kutoka: Tume ya Uchaguzi ya Australia, 1990 Takwimu za Uchaguzi, AEC, Canberra.
AV {Alternative Voting]