Huku mfumo wa List PR ukiegemezwa kwenye kanuni kwamba vyama au makundi ya kisiasa hutoa wagombeaji, kuna uwezekano wa kupata wapigaji kura wa kiwango fulani cha uteuzi kwenye list PR kati ya wagombeaji walioteuliwa pamoja na kati ya vyama. Kimsingi kuna teuzi tatu anbazo huweza kuchaguliwa – orodha wazi, funge na huru.
Mifumo mingi ya List PR duniani huwa funge, yaani orodha hiyo huwa imefungwa na chama chenyewe na wapigaji kura hawawezi kueleza upendeleo kwa mgombeaji mahsusi. Mfumo wa List PR uliotumika Afrika Kusini ni mfumo mzuri wa orodha funge. Karatasi ya kura huwa na majina na ishara za vyama, pamoja na picha ya kiongozi wa chama lakini huwa hakuna majina ya wagombeaji binafsi. Wapigaji kura huchagua tu chama wanachopendelea; wagombeaji huwa wameamuliwa mapema na vyama vyenyewe. Hili linamaanisha kuwa vyama vinaweza kujumuisha wagombeaji (labda wanachama kutoka makundi ya makabila madogo au wanawake) ambao huweza kupata shinda ya kupata kuchaguliwa. Kipengele hasi cha orodha funge ni kuwa wapigaji kura hawana nafasi katika kuamua ni nani atakayewakilisha chama. Orodha funge pia huwa hazitoi majibu kwa mabadiliko ya haraka katika matukio. Huko Ujerumani Mashariki, katika uchaguzi wa kabla ya muungano wa mwaka wa 1990, mgombeaji aliyetangulia katika orodha ya chama kimoja alitambuliwa kama mtoa habari wa askari wa siri siku nne tu kabla ya uchaguzi na papo hapo akafurushwa kutoka kwenye chama; lakini kwa sababu orodha zilikuwa funge, wapigaji kura hawakuwa na namna ila kumchagua ikiwa walitaka kuunga mkono chama cha awali.
Mifumo mingi ya List PR huko Uropa Magharibi hutumia orodha wazi ambapo wapigaji kura huweza kuonyesha sio tu chama wanachopenda bali mgombeaji wampendao katika chama. Katika mingi ya mifumo hii, kura kwa mgombeaji pamoja na chama huwa ya hiari na kwa sababu wapigaji kura wengi huwekea vyama pekee alama kwenye karatasi za kura kuliko kwa wagombeaji, nafasi ya mgombeaji waliyemteua katika karatasi ya kura kawaida huwa na athari kidogo. Hata hivyo, huko Sweden , zaidi ya asilimia 25 ya wapigaji kura kawaida huchagua mgombeaji pamoja na chama, na huchaguliwa ambao hawangekuwa kwenye orodha kama ingekuwa funge.
Huko Brazil na Finland, wapigaji kura hulazimika kupigia kura wagombeaji: idadi ya viti vilivyopokelewa na kila chama huamuliwa na idadi kamili ya kura zilizoshindwa na wagombeaji wake, na mpangilio ambao wagombeaji wa chama huchaguliwa kwenye viti hivi huamuliwa kwenye viti hivi huamuliwa na idadi ya kura binafsi watakazopata. Huku hili likiwapa wapigaji kura uhuru mwingi zaidi kuhusu uteuzi wao wa mgombeaji, pia huwa na athari ambazo hazipendezi. Kwa sababu wagombeaji kutoka chama kimoja huwa wanashindania kura wenyewe, mfumo huu wa orodha wazi huweza kupelekea kuwepo kwa migogoro na migawanyiko katika chama. Pia humaanisha kwamba faida zinazowezekana katika chama za kuwa na orodha zinazoonyesha rekodi ya wagombeaji anuwai huweza kupinduliwa. Katika uchaguzi wa orodha wazi ya PR huko Sri Lanka, kwa mfano, majaribio ya vyama vikuu vya Sinhalese kujumlisha wagombeaji wachache wa Tamil katika nafasi zinazoweza kushinda kwenye orodha yao ya chama zimechukuliwa kama ambazo haziwezi kufanya kazi kwa sababu wapigaji kura wengi walichagua kimakusudi, wagombeaji wa viwango vya chini wa Sinhalese badala ya hao wengine. Huko Kosovo, badiliko kutoka orodha funge hadi orodha wazi liliwezesha uwepo wa wagombeaji zaidi waliozidi. Kwa kufuata mtazamo huo, orodha wazi wakati mwingine huonekana kama zenye kutopendelea uwakilishaji wa wanawake katika jamii zenye mielekeo ya uume, hata kama huko Poland wapigaji kura wameonekana kuwa tayari kutumia orodha wazi kuchagua wanawake zaidi kuliko ambavyo ingetokea kutokana na uteuzi ambao ungefanywa na vyama ikiwa orodha funge zingetumika.
Vyombo vingine hutumiwa katika idadi ndogo ya utawala ili kuongeza matumizi zaidi ya mifumo ya orodha wazi. Huko Ecuador, Luxembourg na Switzerland, wapigaji kura huwa na kura nyingi kama vilivyo viti vya kujazwa na huweza kuvigawa kwa wagombeaji ama ndani ya orodha ya chama kimoja au kwenye orodha ya vyama kadhaa kulingana na wanavyopendelewa. Uwezo wa kupigia kura zaidi ya mgombeaji mmoja kwenye orodha tofauti ya chama (inayojulikana kama panachage) au kupiga kura zaidi ya moya kuchagua mgombeaji mmoja anayependelewa zaidi (inayojulikana kama cumulation) vyote hutoa kipimo zaidi cha udhabiti kwa mpigaji kura na huorodheshwa hapa kama mifumo ya orodha wazi.

