Chini ya mifumo ya MMP, viti vya PR hutolewa ili kufaidi ukosefu wowote wa uwakilishaji unaotokana na matokeo ya viti vya wilaya. Kwa mfano ikiwa chama kimoja kitashinda asilimia 10 ya kura nchini lakini kikose kupata viti wilayani, basi kitapewa viti vya kutosha kutokana na orodha ya PR ili kupandisha uwakilishaji wake hadi asilimia 10 ya viti vyote bungene. Kura zinaweza kupata teuzi mbili tofauti kama ilivyo huko Ujerumani na New Zealand. Kwa upande mwingine, wapigaji kura huweza kufanya uteuzi mmoja tu huku idadi kamili ya chama ikitolewa kutokana na idadi kamili zote za wagombeaji kutoka kila wilaya .
Kiwango cha elementi hizi mbili za mfumo huwa tofauti kutoka nchi moja hadi nyingine. Mfumo wa uchaguzi wa baada ya machafuko huko Lesotho huwa na viti 80 vya FTPT na viti 40 vya kufidiwa huku Ujerumani wakichagua wagombeaji 299 chini ya kila mfumo.
Hata kama mfumo wa MMP umepangwa ili kutoa matokeo yaliyosawazishwa, inawezekana kuwa ukosefu wa usawazishaji katika matokeo ya wilaya yenye uanachama mmoja huwa kubwa kiasi kwamba orodha ya viti haiwezi kuifaidi. Hili huwezekana zaidi wakati wilaya za uchaguzi wa PR huelezewa sio katika kiwango cha kitaifa lakini katika kiwango cha kimaeneo au kimkoa. Chama huweza kushinda viti zaidi vyenye wafuasi wengi kutoka eneo au mkoa mmoja kuliko kura yake ya chama kutoka eneo hilo ambazo ilikuwa ipate. Ili kushughulikia hili usawazishaji huweza kutazamwa kwa karibu ikiwa ukubwa wa bunge utaongezeka kwa kiasi: viti vya zaidi huitwa mamlaka yanayojitokeza au uberhangsmandaten. Hili limewahi kutokea katika uchaguzi mwingi huko Ujerumani na pia huweza kutokea huko New Zealand. Huko Lesotho, ikilinganuliwa, ukubwa wa bunge huwa funge na matokeo ya uchaguzi wa kwanza wa MMP mwaka wa 2002 hayakuwa na usawazishaji kamili.
Jedwali la 4 Nchi zinazotumia Mifumo ya MMP


