Idadi fulani ya jamii mbalimbali kikabila imechukua dhana ya viti vilivyotengwa katika upanuzi wao wa kimantiki. Viti havijagawanywa tu kutegemea misingi ya pamoja, lakini mfumo wote wa uwakilishaji bungeni una misingi kama hiyo ya mitazamo ya pamoja. Kuna orodha tofauti ya wapigaji kura kwa kila jamii bainifu ambayo huchagua wanachama kutoka ‘kundi lao pekee’ ili kuingia bungeni.
Huko Lebanon, wilaya zenye wanachama zaidi ya mmoja hubainishwa, ambapo katika kila mojawapo ugawaji wa viti kati ya makundi yalioungana hubainishwa. Wawakilishi huchanganuliwa kwa kutumia mfumo wa Block Vote kutokana na orodha ya pamoja kwa njia tofauti katika viti vilivyotengewa kila kikundi kilichoungana . Huko Fiji, wapigaji kura wa pamoja, wanapohakikisha uwakilishaji wa kikundi kawaida huwa na athari za kupotosha za kupuzilia mbali mwelekeo wa kukubali kati ya makundi tofauti, kwa kuwa hakukuwa na vichocheo vya kisiasa vilivyopatikana katika ya jamii. Majukumu ya kumbainisha mwanachama kutoka kundi fulani na kugawa viti kwa usawa kati yao yalikuwa pia na matatizo huko India , kwa mfano, wilaya tofauti ambazo zilikuwepo chini ya uongozi wa kikoloni wa Waislamu, Wakristo, Wasikh na wengine zilifutiliwa mbali wakati wa kupata uhuru, hata kama baadhi ya viti vilivyotengwa vilisalia ili kuwakilisha makabila na matabaka yaliyopangwa. Mifumo ya orodha ya pamoja iliyotumiwa katika nyakati mbalimbali huko Paksistan, Cyprus, na Zimbambwe pia imetupiliwa mbali. Licha ya historia yenye mabishano ya matumizi yake, Fiji huendelea kuchagua sehemu ya wanabunge wake kutokana na orodha ya pamoja iliyo tofauti katika kuwachagua watu wa asili ya Fiji, India, Rotuman na wapigaji kura ‘kwa jumla’.
Huku baadhi ya mipango ya orodha za pamoja ikitoa jukumu la kuamua ni nani atakayekuwa katika kategoria gani ya aina fulani ya taasisi ya usajili, wengine hutolea watu binafsi uteuzi huu. Mfano unaojulikana zaidi wa mfumo wa orodha ya pamoja unaotumika sasa miongoni mwa demokrasia za kisiasa ni orodha iliyo tofauti ya hiari inayotumika kwa wapigaji kura wa Maori huko NewZealand. Wapigaji kura wa Maori huweza kuchagua kuwa katika ama kwenye orodha ya uchaguzi ya kitaifa au kuwa kwenye orodha mahususi ya Maori, ambayo sasa huchagua wawakilishaji saba bungeni kutoka Maori. Matokeo ya uchaguzi wa kwanza wa PR huko New Zealand tangu mwaka wa 1996 huweza, hata hivyo, kuelezwa kama wenye kudhoofisha mitazamo ya mfumo wa pamoja: wawakilishaji mara mbili wa Maori wamewahi kuchaguliwa kutokana na orodha ya kijumla kama ilivyo katika orodha mahsusi ya Maori.

