Habari Mahususi na Majukumu ya Elimu
Maafisa wa uchaguzi watateua wafanyikazi kusimamia na kuendeleza mipango ya elimu na habari kwa Wapigakura kwa niaba ya wasimamizi wa uchaguzi. Mpangilio wa afisi hizi huenda ukategemea hali ya mamlaka ya kusimamia uchaguzi, kama vile, Je, ni ya kudumu au ni ya muda, upeo wa jukumu la kisheria la mamlaka ya kusimamia uchaguzi kuendeleza elimu kwa Wapigakura na / au vigezo vya Mpango husika. Mpangilio wa wafanyikazi pia utategemea na ikiwa au la Mpango unaendelezwa kwa ajili ya uchaguzi mahususi au kama sehemu ya Mpango wa kura kwa raia na / au Wapigakura unaoendelea na ikiwa au la unawalenga wanaostahili kupiga kura au pia unahusisha watoto.
Katika hali yoyote ile, kutakuwa na wafanyikazi ambao watakuwa na jukumu mahususi la kutoa elimu na habari kwa Wapigakura. Pia kutakuwa na wafanyikazi, ambao watawajibikia uhusiano na vyombo vya habari, utoaji mafunzo kwa maafisa na wafanyikazi wengine wa kuendesha uchaguzi, na ambao wanashughulikia usimamizi wa mahusiano na umma. Hatimaye, kutakuwa na makamishna na maafisa wa ngazi za juu wa mamlaka ya kusimamia uchaguzi ambao pia watakuwa na jukumu la mawasiliano na umma.
Uratibu wa mawasiliano na ukuzaji wa Mpango wa elimu litakuwa jukumu muhimu la mamlaka ya kusimamia uchaguzi. Waelimishaji wanafaa kuwa na jukumu katika haya na sio waonekane tu kama watendaji wa shughuli za kiofisi. Kila jambo ambalo utawala wa kusimamia uchaguzi wanaeleza lina athari kwa mitazamo, michukulio, na ufahamu wa Wapigakura. Usimamizi mzuri wa maelezo au taarifa hizi unawezesha wasimamizi kupunguza uharibifu wa malighafi na juhudi za bure.
Kwa kweli, wasimamizi wa kitaifa wa uchaguzi ni sehemu moja tu ya ngazi za utawala wa uchaguzi. Kwa kutegemea jinsingazi hizo (za kiutawala) zilivyoendelea na wingi wa malighafi waliyonayo, kunaweza kuwa na waelimishaji, maafisa wa kusimamia mahusiano na umma, na wanaotoa mafunzo katika viwango vya chini vya tume ya uchaguzi. Uwezo wa kuthibiti maingiliano na mawasiliano yao utakuwa muhimu.
Athari za Mienendo Katika Shirika na Katika Umma
Mpango wa elimu, hata hivyo, unafaa kutazamwa katika muktadha mpana. Kila afisa ambaye anahusika na usimamizi wa uchaguzi ana jukumu la kutekeleza katika uelimishaji wa umma. Kwa kweli, wanafanya hivi hata kama hawatarajii kufanya. Mienendo yao katika kushughulikia umma wakati wa usajili wa Wapigakura, kushughulika malalamiko na kusimamia maeneo ya kupigia kura inaweza kuwa ya kielimu au inaweza kuhujumu ari za Wapigakura. Litakuwa jambo muhimu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha kuwa mienendo yao kila wakati haiegemei au kupendelea nani ya kitaalamu, na kuwa inaendana na ujumbe kwa umma ambao unatolewa kuhusu uchaguzi na kuhusu mamlaka ya kusimamia chaguzi yenyewe.
Mbali na kanuni hii ya kijumla- ambayo inaweza kuchukuliwa kama sifa ya ndani ya mamlaka ya kusimamia uchaguzi – pia kuna jukumu lingine muhimu la kielimu ambapo maafisa wote wanaweza kushiriki. Na wanafaaa kupokea mafunzo na habari za kutosha ili waweze kutekeleza jukumu hili kikamilifu. Ili haya yaweze kufaulu, mafunzo na habari zafaa kutayarishwa katika wakati ufaao.
Pamoja na habari zitolewazo kwa wakati ufaao, uteuzi wa mapema wa wafanyikazi wa kuendesha shughuli halisi ya uchaguzi na maafisa wa kusimamia uchaguzi katika maeneo mbalimbali, utahakikisha kuwa kuna watu katika jamii za mashinani ambao wanajihusisha na mchakato wa uchaguzi na hivyo wanaweza kuwa chanzo cha habari kwa Wapigakura wanaoishi karibu nao.
Maafisa Wa Uchaguzi Kama Waelimishaji
Kwa kawaida, huwa kuna njia mbili ambazo maafisa wanaweza kuwashughulikia wateja wao. Wanaweza kujifanya kana kwamba wateja lazima wajue au watafute habari wanazozihitaji ili waweze kupata huduma. Auwanawezakuwapa, aidha kwa njia ya mazungumzo ya mdomo au kupitia kwa habari njema na zenye saini, pamoja na ufahamu ambao wateja wao wanahitaji.
Inawezekana kuwa haya yanaweza kufanywa katika kiwango chochote katika mchakato wa uchaguzi, hata katika maingiliano yao na Wapigakura katika kituo cha kupigia kura. Bila shaka, ikiwa maafisa hawapewi mafunzo ya kufanya kazi yao lakini pia wanapewa na kufahamishwa kuhusu vijitabu vyenye maelezo ya elimu kwa Wapigakura au seti ya maswali yanayoulizwa mara kwa mara, wanaweza kusaidia sana Mpango waelimu kwa Wapigakura.