Baada ya miaka mingi ambayo demokrasia zilizohimarika zimetumia kiamilifu katika mienendo na taasisi ili kuhimili uraia wa kidemokrasia, hofu za hivi karibuni kuhusu matendo yasiyo demokrasia yanayoibuka, makundi yaliyotenganishwa, na Wapigakura wasiojali yamesababisha kuibuka kwa mjadala mkali kuhusu juhudi zaidi, ambazo baadhi yazo ni za kielimu na zingine kupitia kwa majaribio katika mabadiliko ya kiuchaguzi, na uimarishaji upya wa vyama na demokrasia ya moja kwa moja.
Wakati mwingine huwa inasahaulika kuwa demokrasia zilizohimarika zina historia yake ya mizozo na mafadhaiko. Baadhi ya taasisi, tamaduni na taratibu ambazo zinapatikana zilitokana na nyakati za mfadhaiko na zinajiimarisha zenyewe baadaye wakati matatizo sawa na hayo yanapoibuka. Matatizo mengine yanayozikabili jamii hizi yanaweza kuwa mapya na hivyo kuhitaji taasisi mpya.
Katika Mataifa ya Marekani, mtalaa wa elimu kwa raia umeundwa kwa matumizi katika shule za umma, na Mpango kama huo pia umekuwepo katika Uingereza. Mipango hii yote iliibuka nje ya mfumo rasmi wa serikali na ulitegemea ushawishi, utetezi na kazi iliyofanywa na shule na walimu binafsi kuhamasisha ukubalifu wake kwa wingi.
Nchini Ujerumani, mashirika na vyuo vya kawaida ambavyo viliibuka katika miaka ya 1950 baada ya vita kuamsha uraia na kuhakikisha kuwa kulikuwa na maridhiano na ujenzi vinaendelea kufanya kazi katika mfumo wa kisiasa unaohimiliwa na serikali za kitaifa (kimajimbo) na mawakala wa serikali za wilaya.
Wakati Uropa imepanuka na kuwa changamano, mipango ya elimu ya Muungano wa Ulaya, ikiwa pamoja na ile ya kutoa habari na iliyo na lengo la kindani la kielimu imeanzishwa. Mfumo mtandao chini ya mradi wa Grundtvig / Socrateshutoa habari na mafunzo yafaayo. Kuibuka kwa majukumu ya raia ya kimpito yanamaanisha changamoto mpya kwa waelimishaji.
Bila shaka katika jamii changamano zaidi kama hizo kama zilizoibuka kutokana natamaduni zilizoimarika na za siku nyingi, ni vigumu kwa waelimishaji kuwazia mipango ya kilimwengu, na michache ya mipango hii inapatikana. Wale ambao wanataka kuanzisha mipango kama hiyo kwa ajili ya nyakati maalum za kidemokrasia watapata usaidizi katika sehemu za usawazishaji na mikakati. Badala ya hayo, waelimishaji wanafanya kazi na wahamiaji wapya, makundi yaliyotengwa, uimarishaji wa vyama vya kisiasa, kuendeleza kampeni za haki za kibinadamu na ukuzaji wa elimu.
Baadhi ya nchi, hasa zile zilizo na historia ya kimishonari au kikoloni zimetumia maendeleo ya elimu kuwazindua wananchi wao kwa hatua za nyumbani na ushikamano na kimataifa na huruma wa kimataifa. Mbinu zinazotumika katika kampeni hizi zinafaa kuchunguzwa vizuri ili kuhakikisha hazileti tu umoja wa kijamii wa muda mfupi bila ya kuambatanishwa na uzingatifu wa kudumu kwa demokrasia na raia wenye bidii.